Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo Lampard kuwashiwa taa ya kijani Chelsea
Michezo

Lampard kuwashiwa taa ya kijani Chelsea

Frank Lampard
Spread the love

 

TAARIFA kutoka vyanzo mbalimbali nchini Uingereza vinasema huwenda muda wowote klabu ya Chelsea ikamtimua kocha wake wa sasa Frank Lampard kufuatia matokeo mabovu ya hivi karibuni na nafasi yake itachukuliwa na kocha wa zamani wa PSG, Thomas Tuchel. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Tuchel ambaye pia alikuwa kocha wa zamani wa klabu ya Borrusia Dortmund taarifa zinaeleza kuwa tayari yupo kwenye mazungumzo na mabosi wa klabu ya Chelsea kuja kuchukua mikoba ya Lampard ambaye muda wowote ataondoka klabuni hapo.

Lampard ambaye ni mchezaji wa zamani wa timu ataondoka kwenye klabu hiyo kutokana na kuwa na mwenendo mbovu wa matokeo kwenye michezo ya Ligi Kuu nchini England.

Mpaka sasa Lampard ameingoza Chelsea kwenye michezo 83 katika kipindi cha miezi 18, toka alipojiunga na klabu hiyo msimu uliopita.

Mpaka sasa Chelsea ipo nafasi ya tisa kwenye msimamo wa Ligi hiyo mara baada ya kucheza michezo 19 na kufanikiwa kuibuka na ushindi kwenye michezo nane, huku akipoteza mechi sita na kwenda sare michezo mitano.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!