Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mafunzo ya kujitolea JKT 2020/21 yasitishwa
Habari Mchanganyiko

Mafunzo ya kujitolea JKT 2020/21 yasitishwa

Spread the love

JESHI la Kujenga Taifa (JKT) nchini Tanzania, limesitisha mafunzo ya JKT kundi la kujitolea kwa mwaka 2020-2021. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Kutokana na usitishwaji wa mafunzo hayo, limewataka vijana ambao walikuwa bado hawajaripoti wasiende kuripoti katika makambi waliyopangiwa mpaka hapo itakapotangazwa tena na wale ambao wamefika warejee nyumbani.

Hayo yameelezwa leo Jumanne tarehe 19 Januari 2021 na Kaimu Mkuu wa Utawala JKT, Kanali Hassan Mabena alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma.

Kanali Mabena amesema, mafunzo hayo yalikuwa yaanze hivi karibuni katika makambi mbalimbali nchini hivyo wameyasitisha kwa muda mpaka hapo itakapotangazwa.

Amesema kutokana na kusitishwa kwa mafunzo hayo, JKT inawataka vijana wote ambao walichaguliwa na kuripoti makambini kwa ajili ya kuhudhuria mafunzo ya JKT ya kujitolea warejee majumbani kwao.

Kanali Mabena amesema na wale ambao walikuwa bado hawajaripoti wasiende kuripoti katika makambi waliyopangiwa mpaka hapo itakapotangazwa tena.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

Polisi wakanusha kufanya uzembe ajali iliyouwa mwandishi Ayo Tv

Spread the loveJESHI la Polisi limekanusha tuhuma zilizoibuliwa dhidi yake  kwamba limekawia...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

Habari Mchanganyiko

GGML yaja na teknolojia za kisasa maonesho ya OSHA Arusha

Spread the loveKATIKA kuelimisha wananchi na washiriki wa maonesho ya usalama na...

error: Content is protected !!