JESHI la Kujenga Taifa (JKT) nchini Tanzania, limesitisha mafunzo ya JKT kundi la kujitolea kwa mwaka 2020-2021. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).
Kutokana na usitishwaji wa mafunzo hayo, limewataka vijana ambao walikuwa bado hawajaripoti wasiende kuripoti katika makambi waliyopangiwa mpaka hapo itakapotangazwa tena na wale ambao wamefika warejee nyumbani.
Hayo yameelezwa leo Jumanne tarehe 19 Januari 2021 na Kaimu Mkuu wa Utawala JKT, Kanali Hassan Mabena alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma.
Kanali Mabena amesema, mafunzo hayo yalikuwa yaanze hivi karibuni katika makambi mbalimbali nchini hivyo wameyasitisha kwa muda mpaka hapo itakapotangazwa.
Amesema kutokana na kusitishwa kwa mafunzo hayo, JKT inawataka vijana wote ambao walichaguliwa na kuripoti makambini kwa ajili ya kuhudhuria mafunzo ya JKT ya kujitolea warejee majumbani kwao.
Kanali Mabena amesema na wale ambao walikuwa bado hawajaripoti wasiende kuripoti katika makambi waliyopangiwa mpaka hapo itakapotangazwa tena.
Leave a comment