Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Mafunzo ya kujitolea JKT 2020/21 yasitishwa
Habari Mchanganyiko

Mafunzo ya kujitolea JKT 2020/21 yasitishwa

Spread the love

JESHI la Kujenga Taifa (JKT) nchini Tanzania, limesitisha mafunzo ya JKT kundi la kujitolea kwa mwaka 2020-2021. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Kutokana na usitishwaji wa mafunzo hayo, limewataka vijana ambao walikuwa bado hawajaripoti wasiende kuripoti katika makambi waliyopangiwa mpaka hapo itakapotangazwa tena na wale ambao wamefika warejee nyumbani.

Hayo yameelezwa leo Jumanne tarehe 19 Januari 2021 na Kaimu Mkuu wa Utawala JKT, Kanali Hassan Mabena alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma.

Kanali Mabena amesema, mafunzo hayo yalikuwa yaanze hivi karibuni katika makambi mbalimbali nchini hivyo wameyasitisha kwa muda mpaka hapo itakapotangazwa.

Amesema kutokana na kusitishwa kwa mafunzo hayo, JKT inawataka vijana wote ambao walichaguliwa na kuripoti makambini kwa ajili ya kuhudhuria mafunzo ya JKT ya kujitolea warejee majumbani kwao.

Kanali Mabena amesema na wale ambao walikuwa bado hawajaripoti wasiende kuripoti katika makambi waliyopangiwa mpaka hapo itakapotangazwa tena.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!