Thursday , 9 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa RC K’njaro ataka ‘spidi’ ujenzi wa madarasa
Habari za Siasa

RC K’njaro ataka ‘spidi’ ujenzi wa madarasa

Anna Mghwira, Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro
Spread the love

ANNA Mghwira, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ameagiza watendaji na wakurugenzi wa mkoa huo kuhakikisha wanakamilisha ujenzi wa madarasa mapema ili wanafunzi waliochaguliwa kuanza Kidato cha Kwanza, wasikose nafasi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kilimanjaro…(endelea).

Ametoa kauli hiyo kwenye kikao maalum cha kujadili changamoto ya uhaba wa madarasa na kwamba, katika wilaya za Hai, Moshi Vijijini, Siha na Same wanakabiliwa na uhaba wa madarasa yapatayo 60.

“Wanafunzi 2,900 hawataweza kuendelea na masomo ya Kidato cha Kwanza ambapo Hai wataishindwa kuendelea ni 890, Moshi Vijijini 350, Same 1,414 na Siha 305,” amesema Mghwira.

Pia amemtaka Ofisa Elimu wa Mkoa, Paulina Mkwama kuhakikisha anarekebisha Ikama ya Walimu katika baadhi ya wilaya kutoka na upungufu mkubwa wa walimu unaokabili mkoa huo.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

error: Content is protected !!