Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa ACT-Wazalendo wamlilia Askofu Banzi
Habari za Siasa

ACT-Wazalendo wamlilia Askofu Banzi

Zitto Kabwe, Kiongozi Mkuu wa ACT-Wazalendo
Spread the love

CHAMA cha ACT-Wazalendo, kimetuma salamu za pole kufuatia kifo cha Askofu wa Jimbo la Katoliki Tanga, Anthony Banzi. Anaripoti Mwandishi wetu… (endelea).

Askofu Banzi amefariki leo tarehe 20 Disemba 2020, katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MHN) alipokiwa amelazwa kwa ajili ya matibabu.

Taarifa za kifo cha Askofu Banzi zilitolewa na Padre Charles Kitima, Katibu Mkuu wa Baraza Katoliki la Maaskofu Tanzania (TEC) mapema leo asubuhi na kueleza kuwa tarehe ya mazishi itatolewa baadaye.

“Baraza la Maaskofu Tanzania linasikitika kutangaza kifo cha Baba Askofu Anthony Banzi wa Jimbo la Katoliki Tanga, amefariki leo tarehe 20 Disemba 2020 na tarehe ya mazishi tutajulishwa baadaye,” ilieleza taarifa hiyo.

Kufuatia kifo hicho, Chama cha ACT-Wazalendo kimetuma salamu zake za rambirambi kupitia kwa Janeth Rithe, Naibu Katibu wa Habari, Uenezi na Mahusiano kwa Umma wa chama hicho na kimeeleza kusikitishwa na taarifa hizo za kifo.

Amesema, chama hicho kinatoa pole kwa familia ya Askofu, ndugu na jamaa na kuwataka kuwa na subira katika wakati huu wa msima.

“Chama cha ACT-Wazalendo kimehuzunishwa na taarifa ya kifo cha Baba Askofu Anthony Banzi wa Jimbo la Katoliki la Tanga kilichotokea leo tarehe 20 Disemba 2020 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

“Katika uhai wake, Baba Askofu Banzi amelitumikia Taifa kiroho kwa upendo mkubwa. Chama cha ACT-Wazaleno kinatuma salamu za pole kwa kanisa la Katoliki Jimbo la Tanga, kwa wakatoliki wote na watu wote walioguswa kwa namna moja ama nyingine, Mungu awape faraha katika kipindi hichi kigumu,” imeeleza taarifa hizo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!