Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Waziri Aweso awasimamisha watatu DDCA, atoa maagizo Dawasa
Habari za Siasa

Waziri Aweso awasimamisha watatu DDCA, atoa maagizo Dawasa

Juma Aweso, Waziri wa Maji
Spread the love

WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewasimamisha kazi watumishi watatu wa Wakala wa Uchimbani Visima (DDCA) kutokana na tuhuma za ubadhilifu na kuagiza uchunguzi dhidi yao ufanyike. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea)

Pia, ameiagiza Mamlaka ya Majisadi na Usafi wa Mazingira (Dawasa) kuongeza mikoa ya kihuduma ili kuhakikisha inasogeza huduma kwa wananchi.

Waliosimamishwa ni; Abdallah Abdulhaman (Kitengo cha Ufundi), Fadhir Sauko (Kitengo cha Utafiti wa maji ardhini) na Hamad Msuwa wa Kitengo cha Manunuzi.

Aweso amechukua uamuzi huo leo Jumatatu tarehe 14 Desemba 2020 alipofanya ziara ya kutembelea miradi ya maji mikoa ya Dar es Salaam na Pwani.

Amemuagiza Katibu Mkuu, Wizara ya Maji,Mhandisi Antony Sanga kufanya uchunguzi wa tuhuma za Chuo cha Maji kuhusu uuzwaji wa nyumba za chuo kinyume na utaratibu ili hatua zaidi ziweze kuchukuliwa dhidi yao.

Awataka watendaji waliopo chini ya Wizara ya Maji, kufanya kazi kwa kufuata misingi na kanuni za utumishi wa umma.

Aweso ameahisi kutowafumbia macho watumishi wasio waaminifu.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Dawasa, Mhandisi Cyprian Luhemeja

Kuhusu Dawasa, amesema ili kuwafikia wananchi karibu zaidi ni lazima kuongeza mikoa ya kihuduma.

Kwa sasa, Dawasa ina mikoa 15 ya kihuduma ikiwa ni mamlaka ya maji kubwa kuliko zote nchini Tanzania ikiwa inaongoza pia katika ukusanyaji wa mapato.

“Mnafanya kazi nzuri Dawasa kwa kusimamia vyema miradi ya maji kwa ufanisi na kuleta matokeo makubwa kwa haraka zaidi, lakini ongezeni mikoa ya kihuduma ili kuwasogezea wananchi huduma,” amesema Aweso

Aweso ameitaka Dawasa kuhakikisha Mradi wa Maji Mkuranga -Vikindu unakamilika kabla ya muda wa mkataba ambao ni Februari 2021 ili wananchi waanze kupata huduma ya majisafi.

Waziri huyo ameahidi kuwalipa wakandarasi kwa wakati ili mradi uweze kumalizika mapema huku akiipongeza
kampuni ya Shanxi Construction Engineering kwa kukamilisha ndani ya wakati.

Agizo jingine ambalo Aweso amelitoa ni kuitaka Dawasa kukaa pamoja na ofisi ya bonde la maji Wami ili kupata eneo kubwa zaidi kwa ajili ya kulinda chanzo cha Maji kwa Mji wa Mkuranga.

Kwa upande wake, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Dawasa, Mhandisi Cyprian Luhemeja amemuahisi Waziri Aweso kutekeleza maagizo yake ili kusogeza huduma kwa wananchi kwa kasi zaidi.

Mhandisi Luhemeja amesema, wanaendelea kutekeleza miradi mbalimbali kwa fedha za mapato ya ndani ili kuhakikisha wananchi wanapata majisafi kwa wingi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!