Saturday , 25 March 2023
Home Kitengo Michezo Azam Fc hali tete, yabanwa mbavu na Namungo
Michezo

Azam Fc hali tete, yabanwa mbavu na Namungo

Kikosi cha timu ya Namungo FC
Spread the love

BAO la dakika ya 90 +4 la Steven Sey lilitosha kuipatia Namungo sare kwenye mchezo dhidi ya Azam FC, katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliomalizika kwa sare ya mabao 2-2 na kuifanya Azam FC kucheza mchezo wa sita bila kupata ushindi. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo huo ulichezwa kwenye uwanja wa  Azam Complex, Chamazi mbele ya kicha wake mpya, George Lwandamina akiiongoza timu hiyo kwa mara ya kwanza tangu alipopewa kibarua cha kuinoa mara baada ya kutimuliwa kwa Aristica Cioaba.

Azam ilikuwa ya kwanza kutangulia kwenye mchezo huo baada ya kupachika bao la kwanza lililofungwa na Iddi Nado dakika ya 19 na dakika tano baadae beki wa kushoto wa Namungo Edward Manyama alichomoa bao hilo kwenye dakika ya 24 kwa mpira wa adhabu ndogo na kufanya timu hizo kwenda mapumziko zikiwa zimetoshana nguvu.

Dakika ya 74 kipindi cha pili, Nado aliiandikia Azam bao la pili huku timu hiyo ikiwa na matumaini ya kuondoka na pointi tatu ndipo Steve Sey mshambuliaji raia wa Uganda aliipachikia Namungo bao la kusawazisha baada ya kuunganisha kona iliyopigwa na Lucas Kikoti kwenye dakika ya 90+4.

Prince Dube

Kwa matokeo hayo Azam itasalia kwenye nafasi ya tatu ikiwa na pointi 28 baada ya kucheza michezo 15, ikiwa nyuma kwa pointi moja dhidi ya Simba ambayo imecheza michezo 13, huku Yanga akiendelea kusalia kileleni akiwa na pointi 37 na michezo 15.

Namungo imepanda mpaka nafasi ya 13 ikiwa na pointi 17 baada ya kucheza michezo 13 na mechi mbili mkononi.

Mchezo ujao wa Ligi Azam itashuka dimbani dhidi ya Ruvu Shooting ambayo inashika nafasi ya nne kwenye msimamo ambayo ilicheza michezo saba bila kupoteza kabla ya kufungwa na Yanga kwa mabao 2-1.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

Michezo

Kimwanga CUP yazidi kutimua vumbi

Spread the loveMASHINDANO ya mpira wa miguu ya Kimwanga CUP ya kuwania...

error: Content is protected !!