Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Ndugai awaapisha Polepole, Riziki
Habari za Siasa

Spika Ndugai awaapisha Polepole, Riziki

Aliyekuwa Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai
Spread the love

SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai amewaapisha Humphrey Polepole na Riziki Lulinda kuwa wabunge wa Bunge hilo. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam … (endelea).

Polepole na Riziki wameapishwa leo Jumatatu tarehe 30 Desemba 2020 Viwanja vya Bunge jijini Dar es Salaam.

Wawili hao, wameapishwa baada ya Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli jana Jumapili kuwateua kuwa wabunge katika nafasi zake kumi za wabunge.

Polepole anaingia kwa mara ya kwanza bungeni huku Riziki yeye anarejea kwa mara nyingine kwani katika Bunge lililopita alikuwa mbunge wa viti maalum kupitia Chama Cha Wananchi (CUF).

Mwishoni mwa mkutano wa Bunge la 11, Riziki alitangaza kurejea Chama Cha Mapinduzi (CCM) alikokuwa akihudumu kabla ya kutimkia CUF.

Humphrey Polepole, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM

Akizungumza baada ya kuaoishwa, Riziki amemshukuru Rais Magufuli kwa kumteua pamoja na wananchi wa Lindi kwa maombi yake.

Polepole ambaye pia ni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM amesema, “namshukuru Mungu wa binguni ambaye yeye imempendeza Rais anipe jukumu hili ili kuwasaidia umma wa Watanzania wanapata maendeleo.”

Amesema, “sisi tutamsaidie Rais John Magufuli kutekeleza yale yaliyoahidiwa. Naahidi kuwa mwaminifu na mtiifu na nitakuwa tayari kujifunza.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!