Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Magufuli: Vitambulisho vya machinga kuboreshwa 
Habari za Siasa

Magufuli: Vitambulisho vya machinga kuboreshwa 

Kitambulisho cha Wajasiliamali
Spread the love

JOHN Magufuli, Rais wa Tanzania amesema, vitambulisho vya wajasirimali ‘machinga’ vitaboreshwa zaidi ili kuwawezesha kupata mikopo benki. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Rais Magufuli amesema hayo wakati akihutubia na kuzindua Bunge la 12 leo Ijumaa tarehe 13 Novemba 2020 jijini Dodoma.

Amesema, katika kipindi cha miaka mitano ijayo, vitambulisho vya wajasirimali vilivyokuwa vinatolewa huko nyuma sasa vitaboreshwa zaidi kwa kuweka taarifa muhimu.

“Kwa miaka mitano ijayo, tutaviboresha ikiwemo kuweka picha na taarifa nyingine muhimu kama ilivyo kwenye vitambulisho vya taifa na paspoti.”

Rais John Magufuli

“Hii itawezesha wafanyabiashara watakaotumia vitambulisho hivyo kutambulika ikiwemo kwenye benki na hivyo kupata mikopo ili kukuza biashara zao,” amesema Rais Magufuli

Amesema, hatua hiyo “itawawezesha kukuwa na kutajirika, tunataka wafanyabiashara wadogo wadogo kukuwa na siyo kubaki walivyo”

Miongoni mwa wageni mbalimbali waliohudhulia ufunguzi huo ni Marais wastaafu wa Tanzania; Jakaya Mrisho Kikwete na Ali Hassan Mwinyi na makamu wa rais mstaafu; Ghalib Mohamed Bilal.

Pia, Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi, Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!