Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Magufuli: Vitambulisho vya machinga kuboreshwa 
Habari za Siasa

Magufuli: Vitambulisho vya machinga kuboreshwa 

Kitambulisho cha Wajasiliamali
Spread the love

JOHN Magufuli, Rais wa Tanzania amesema, vitambulisho vya wajasirimali ‘machinga’ vitaboreshwa zaidi ili kuwawezesha kupata mikopo benki. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Rais Magufuli amesema hayo wakati akihutubia na kuzindua Bunge la 12 leo Ijumaa tarehe 13 Novemba 2020 jijini Dodoma.

Amesema, katika kipindi cha miaka mitano ijayo, vitambulisho vya wajasirimali vilivyokuwa vinatolewa huko nyuma sasa vitaboreshwa zaidi kwa kuweka taarifa muhimu.

“Kwa miaka mitano ijayo, tutaviboresha ikiwemo kuweka picha na taarifa nyingine muhimu kama ilivyo kwenye vitambulisho vya taifa na paspoti.”

Rais John Magufuli

“Hii itawezesha wafanyabiashara watakaotumia vitambulisho hivyo kutambulika ikiwemo kwenye benki na hivyo kupata mikopo ili kukuza biashara zao,” amesema Rais Magufuli

Amesema, hatua hiyo “itawawezesha kukuwa na kutajirika, tunataka wafanyabiashara wadogo wadogo kukuwa na siyo kubaki walivyo”

Miongoni mwa wageni mbalimbali waliohudhulia ufunguzi huo ni Marais wastaafu wa Tanzania; Jakaya Mrisho Kikwete na Ali Hassan Mwinyi na makamu wa rais mstaafu; Ghalib Mohamed Bilal.

Pia, Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi, Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!