Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko GGML kujenga bustani ya kisasa Geita
Habari Mchanganyiko

GGML kujenga bustani ya kisasa Geita

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Gabriel akimuonyesha Mkurugenzi Mtendaji wa GGML Richard Jordinson mchoro wa bustani ya kisasa itakayojengwa Geita Mjini, mwiingine ni Meneja Mahusiano wa GGML Joseph Mangilima
Spread the love

WAKAZI wa Mji wa Geita wanafurahia kuwa sehemu ya mradi wa bustani ya kupumzikia inayoanza kujengwa na Kampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) kwa kushirikiana na Halmashauri ya Mji Geita. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Mradi huo uliotengewa bajeti ya Sh.70 milioni kutoka fedha za mfuko wa GGML za uwajibikaji wa Kampuni kwa Jamii (CSR) zinatarajiwa kukamilisha mradi huo kabla ya mwisho wa mwaka 2020.

Akizungumza katika hafla ya kuzindua ujenzi wa bustani hiyo katika kata ya Kalangalala mjini Geita, Mkuu wa Mkoa wa Geita ,Mhandisi Robert Gabriela.

Amesema, GGML kwa kushirikiana na Halmashauri ya Geita Mji inatekeleza mradi huo kupitia fedha CSR kutoka GGML.

Amesema mradi huo unaotekelezwa katika eneo la mita za mraba 4,000 katika kata ya Kalangalala mjini Geita, una lengo la kuwapatia wakazi wa Mji wa Geita fursa ya kuwa na eneo la kufanya shughuli mbalimbali zikiwemo kupumzika, kupunga upepo pamoja na kuepuka kero za joto.

“Lengo letu ni kuona wakazi wa Mji wa Geita wanafika katika eneo hili kufurahia upepo asilia sanjari na kuona mnara maalum wenye kumbukumbu ya Mkoa wa Geita.

“Bustani hii itakuwa kivutio pia kwa vile inajengwa kwa tofali za kuvutia kwenye maeneo yote ya kupitia na sehemu za watu kuketi hali ambayo itashawishi watu wengi zaidi kukaa na kujionea uzuri wa Mji wetu wa Geita,” amesema Gabriel.

Aidha, Mkurugenzi Mtendaji wa GGML, Richard Jordinson amesema kampuni ya GGML imekuwa ikifanya jitihada kubwa kubadilisha muonekano wa jamii ya Mkoa wa Geita kwa kuanzisha miradi endelevu.

“GGML tunajivunia kuwa, wakati tunasherehekea miaka 20 ya uwekezaji wetu ndani ya Mkoa wa Geita mwaka huu, tumefanikiwa kutekeleza miradi mingi yenye tija na matokeo chanya ikiwemo mnara wa makutano ya barabara Mjini Geita, masoko, taa za barabarani, vituo vya afya, shule na barabara za lami,” amesema Jordinson.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

Habari Mchanganyiko

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu wa GGML

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) pamoja na Wakala...

error: Content is protected !!