Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe, Zitto, Lema waachiwa 
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe, Zitto, Lema waachiwa 

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe na wenzao wameachiwa kwa dhamana na Jeshi la Polisi. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea)

Mbowe na wenzake, wameachiwa leo Jumanne tarehe 3 Novemba 2020 baada ya kushikiliwa tangu juzi usiku Jumapili katika Kituo cha Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam.

Viongozi hao walikamatwa jijini Dar es Salaam kwa nyakati tofauti, wakituhumiwa.

         Soma zaidi:-

kuratibu, kuhamasisha na kuwezesha maandamano ya amani yasiyokuwa na kikomo waliyoyatangaza kuanza jana Jumatatu tarehe 2 Novemba 2020, kupinga matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 28 Oktoba mwaka huu.

Mbali na viongozi hao, wengine ni, Godbless Lema, mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Kaskazini na aliyekuwa meya wa manispaa ya ubungo, Dar es Salaam, Boniface Jacob.

Katika ukurasa wa Twitter wa Chadema umeandika “Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wajumbe wa kamati kuu, Lema na Jacob wameachiwa na Jeshi la Polisi Tanzania kwa dhamana.”

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!