Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe, Zitto, Lema waachiwa 
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe, Zitto, Lema waachiwa 

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe na wenzao wameachiwa kwa dhamana na Jeshi la Polisi. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea)

Mbowe na wenzake, wameachiwa leo Jumanne tarehe 3 Novemba 2020 baada ya kushikiliwa tangu juzi usiku Jumapili katika Kituo cha Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam.

Viongozi hao walikamatwa jijini Dar es Salaam kwa nyakati tofauti, wakituhumiwa.

         Soma zaidi:-

kuratibu, kuhamasisha na kuwezesha maandamano ya amani yasiyokuwa na kikomo waliyoyatangaza kuanza jana Jumatatu tarehe 2 Novemba 2020, kupinga matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 28 Oktoba mwaka huu.

Mbali na viongozi hao, wengine ni, Godbless Lema, mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Kaskazini na aliyekuwa meya wa manispaa ya ubungo, Dar es Salaam, Boniface Jacob.

Katika ukurasa wa Twitter wa Chadema umeandika “Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wajumbe wa kamati kuu, Lema na Jacob wameachiwa na Jeshi la Polisi Tanzania kwa dhamana.”

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!