MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe na wenzao wameachiwa kwa dhamana na Jeshi la Polisi. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea)
Mbowe na wenzake, wameachiwa leo Jumanne tarehe 3 Novemba 2020 baada ya kushikiliwa tangu juzi usiku Jumapili katika Kituo cha Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam.
Viongozi hao walikamatwa jijini Dar es Salaam kwa nyakati tofauti, wakituhumiwa.
Soma zaidi:-
kuratibu, kuhamasisha na kuwezesha maandamano ya amani yasiyokuwa na kikomo waliyoyatangaza kuanza jana Jumatatu tarehe 2 Novemba 2020, kupinga matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 28 Oktoba mwaka huu.
Mbali na viongozi hao, wengine ni, Godbless Lema, mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Kaskazini na aliyekuwa meya wa manispaa ya ubungo, Dar es Salaam, Boniface Jacob.
Katika ukurasa wa Twitter wa Chadema umeandika “Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wajumbe wa kamati kuu, Lema na Jacob wameachiwa na Jeshi la Polisi Tanzania kwa dhamana.”
Shinikizo za mabalozi au?