Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mkutano wa Lissu watawanywa kwa mabomu
Habari za Siasa

Mkutano wa Lissu watawanywa kwa mabomu

Spread the love

JESHI la Polisi Mkoa wa Lindi nchini Tanzania, limeutawanya kwa mabomu ya machozi, mkutano wa Tundu Lissu, mgombea urais wa Tanzania kupitia Chadema aliokuwa anaufanya eneo la Somanga. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Mkutano huo, umetawanywa leo Ijumaa tarehe 23 Oktoba 2020, wakati Lissu akiwa jukwaani ameanza kuwahutubia wananchi waliokuwa wamejitokeza kasikiliza.

Kabla ya kutawanya, Lissu alianza kuzungumza kwa kuwashukuru wana Somanga kwa kujitokeza ili kuwaelezea “ujumbe wa ilani ya Chadema ya uhuru, haki na maendeleo ya watu.”

Amesema, wakati wa kutafuta viongozi “ni wakati wa watu kuzungumza na kuzibana midomo.”

Lissu amesema, wamefika eneo hilo baada ya kuandika barua Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuelezea kuomba kufanya mkutano eneo hilo ambalo hakuna mgombea mwinmgine wa urais mkoani humo.

“Tumekuja hapa, lakini kuna watu wanataka kutuzuia, sisi tutazungumza, mwenye kuanzisha fujo aanzishe, mwenye kupiga watu na apige watu, ratiba ya uchaguzi na shughuli zote za mgombea urais, mamlaka inayohusika ni Tume ya Uchaguzi, si mtendaji wa kata, Rais au waziri mkuu,” alisema Lissu

Baada ya kauli hiyo, mabomu ya machozi yalifyatuliwa kuwatawanya wananchi huku Lissu mwenyewe akitulia jukwani, akiendelea kuona kinachoendelea na baadaye aliondoka jukwaani kwenda kwenye helikopita kwa ajili ya mikutano mingine mkoani humo.

Wakati akiondoka, alisikindizwa na wananchi waliokuwa wakiimba ‘rais, rais, rais…”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!