Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Barabara Ruangwa-Kiranjeranje kuwekwa lami
Habari za Siasa

Barabara Ruangwa-Kiranjeranje kuwekwa lami

Spread the love

MJUMBE wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) nchini Tanzania, Kassim Majaliwa amesema, Serikali ya CCM imepanga kujenga barabara ya kutoka Ruangwa hadi Kiranjeranje kwa kiwango cha lami. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Ametoa kauli hiyo leo Ijumaa tarehe 23 Oktoba 2020 wakati akizungumza na wakazi wa vijiji na kata mbalimbali za wilaya ya Ruangwa ambako alipita kumuombea kura mgombea Urais kwa tiketi ya CCM, Rais John Pombe Magufuli na madiwani wote wa kata hizo.

Akizungumza na wakazi hao kwa nyakati tofauti, Majaliwa amesema, barabara hiyo imo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM na tayari Sh.1.2 bilioni zimeshatolewa ili kufanya upembuzi yakinifu na usanifu.

Barabara hiyo itawafanya wakazi hao wasilazimike kupitia Nanganga hadi Lindi wanapotaka kwenda Dar es Salaam.

“Barabara ya kutoka Ruangwa – Nanjilinji – Kiranjeranje ina urefu wa km.120. Barabara hii ukiangalia kwenye ilani yetu, utaikuta iko uk.75. Barabara nyingine ni ya kutoka Ngongo – Mandawa – Namichiga yenye urefu wa km 85 na hii ilipatiwa Sh.800 milioni na kazi ya upembuzi yakinifu imekwishakamilika, sasa kazi iliyobaki ni kutafuta fedha na kuanza ujenzi,” amesema.

Katika hatua nyingine, Majaliwa ambaye ni mbunge mteule wa jimbo la Ruangwa, amesema katika kipindi cha miaka mitano, wilaya hiyo imepokea zaidi ya sh. bilioni 100 kwa ajili ya shughuli za maendeleo.

“Haijawahi kutokea. Tangu wilaya hii ianzishwe mwaka 1995, imekuwa ikipokea fedha za maendeleo kati ya Sh.3 bilioni hadi Sh.4 bilioni tu. Lakini awamu hii tumepokea Sh.49.5 bilioni kwa ajili ya kazi za maendeleo na hivi karibuni Mheshimiwa Magufuli alitoa Sh.59 bilioni kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Nanganga- Ruangwa kwa kiwango cha lami.”

Katika vijiji vyote alivyosimama na kata za Mandawa, Chikundi, Namichiga na Mbekenyera, Majaliwa amewasihi wakazi hao kuwa ifikapo Jumatano ijayo wajitokeze kwa wingi na kupiga kura za ndiyo kwa Dk. Magufuli na madiwani wa CCM.

“Sisi sote ni wana-Ruangwa na kikubwa tunachotaka ni maendeleo, na maendeleo hayachagui chama. Kwani tukijenga barabara, si tutatumia wote? Fanyeni maamuzi sahihi kwa kukichagua Chama cha Mapinduzi na kumpa kura nyingi Dk. John Pombe Joseph Magufuli,” amesisitiza.

Wakati huohuo, Majaliwa ametumia fursa hiyo kuwashukuru wananchi wa Ruangwa kwa kumpitisha bila kupingwa wakati akiwania ubunge wa jimbo hilo. Bado anaendelea na ziara yake kwenye jimbo la Ruangwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!