Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Waziri Kabudi apata ajali
Habari za Siasa

Waziri Kabudi apata ajali

Prof. Palamagamba Kabudi
Spread the love

WAZIRI wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Profesa Palamagamba Kabudi amepata ajali ya gari mkoani Morogoro leo Jumatano tarehe 14 Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Morogoro … (endelea).

Akizungumza nje ya Hospitali ya Rufaa ya Morogoro, Mkuu wa Mkoa huo, Loata Sanare amesema, leo walikuwa na ziara wilayani Kilosa na tayari walikwisha kufika lakini baadaye walipata taarifa  Waziri Kabudi amepata ajali.

Kabudi naye alikuwa anakwenda Kilosa ambako yeye ni mbunge mteule wa Jimbo hilo kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

“Madaktari wamemcheki hana tatizo kubwa sana, anahitaji kupumzika. Niwatoe wasiwasi  wana Kilosa na Watanzania, Mzee Kabudi amepata ajali lakini anaendelea vizuri,” amesema.

Sanare amesema, baada ya mapumziko aliyopewa Waziri Kabudi, watapata maelekezo mengine ya nini cha kufanya.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!