Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea: Hii ndiyo kazi ya kwanza nitaifanya bungeni
Habari za Siasa

Kubenea: Hii ndiyo kazi ya kwanza nitaifanya bungeni

Spread the love

MGOMBEA Ubunge wa Kinondoni kupitia ACT-Wazalendo, Saed Kubenea amesema, akishinda ubunge kipaumbele chake cha kwanza ni kuhakikisha waliovunjiwa nyumba zao mabondenu wanalipwa fidia. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam…(endelea).

Kubenea ameyasema hayo jana Jumatatu tarehe 12 Oktoba 2020 katika mkutano wake wa kampeni alipokuwa akiwahutubia wananchi wa kata ya Kigogo ambayo ni miongoni mwa waliokumbwa na adha ya kuvunjiwa nyumba zao.

“Siendi bungeni kujifunza, nafahamu kila kitu bungeni, mimi nikiingia ajenda yangu ya kwanza ni mabondeni, wananchi wangu waliobomolewa nyumba zao walipwe fidia na wapewe maeneo mapya yenye huduma za jamii sio kuwachukua watu kuwapekeka ambapo hakuna huduma” alisema.

Kubenea alisema, ana uzoefu na nafasi hiyo kwa kuwa amekuwa mbunge kwa miaka mitano kati ya mwkaa 2015-2020 jimbo la Ubungo na anazijua shida za wananchi wa Kinondoni.

“Nimekuwa mbunge kwa miaka mitano, nimekuwa mwandishi wa habari za bunge kwa miaka 17 na nimekuwa Mtanzania ninayetetea haki za watu ambaye ni kimbilio la wanyonge, mnyonge mwenzenu ni mimi nitawatumikia” amesema.

“Jimbo la Kinondoni kuna wagombea wengi, msiharibu kura zenu kwa kupeleka kwa kila mtu, ili tumshinde Abbas Tarimba (mgombea wa CCM) kura zenu nipeni mimi” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

Serikali kuongeza wanufaika mikopo ya elimu ya juu

Spread the loveSERIKALI imesema itaongeza idadi ya wanufaika wa mikopo ya elimu...

ElimuHabari za Siasa

Serikali kufumua mitaala ya vyuo vikuu, ufundi stadi

Spread the loveSERIKALI inakusudia kufanya mapitio katika mitaala na programu za vyuo...

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

error: Content is protected !!