Wednesday , 29 March 2023
Home Kitengo Michezo Bosi GSM kuongoza kamati ya ushindi Taifa Stars
Michezo

Bosi GSM kuongoza kamati ya ushindi Taifa Stars

Ghalib Said Mohammed
Spread the love

RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia amemteuwa Ghalib Said Mohammed kuwa Mwenyekiti wa kamati ya ushindi ya Timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kuelekea mchezo wa kufuzu AFCON dhidi ya Tunisia. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea). 

Ghalib ambaye ni mkurugenzi wa kampuni ya GSM ambao ni wafadhili wa kuu wa klabu ya Yanga ataongoza kamati hiyo ambayo ina wajumbe 13. 

Viongozi wengine wa kamati wa kamati hiyo ni Salim Abdallah ‘Try Again’ ambaye ni makamu mwenyekiti, huku katibu wa kamati hiyo ni Mhandisi Hersi Said ambaye ni mjumbe wa mashindano klabu ya Yanga.

Salim Abdallah ‘Try Again’

Wajumbe walioteuliwa kwenye kamati hiyo ni Abdallah bin kleb, Haji Manara, Jerry Muro, Patrick Kahemele, Zacharia Hanspope, Beatrice Singano, Christina Manyenye, Said Nassor.

Wengine ni Anitha Rwehumbiza, Farid Nahdi, Feisal Abri, Farough Baghozal, Nandi Mwinyimbella na Phelomen Ntahijala.

Taifa Stars inatarajia kucheza mchezo wa kufuzu Kombe la Mataifa Africa, AFCON dhidi ya Tunisia utakaopigwa 13 Novemba, 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

TANROADS wawataka watumishi wazingatie michezo kazini

Spread the love  WAKALA wa barabara Tanzania (TANROADS) imesema michezo inapaswa kuzingatiwa...

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

error: Content is protected !!