Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ‘Mchawi’ wa Mbowe Hai achunguzwa
Habari za Siasa

‘Mchawi’ wa Mbowe Hai achunguzwa

OCD wa Hai akizungumza na mgombea ubunge wa Hai kupitia Chadema, Freeman Mbowe
Spread the love

OFISA wa Jeshi la Polisi katika Jimbo la Hai, Mkoani Kilimanjaro, anachunguzwa na jeshi hilo kwa madai ya kumtabiria Freeman Mbowe, mgombea ubunge wa jimbo hilo kung’olewa kwenye uchaguzi mkuu mwaka huu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kilimanjaro…(endelea).

Taarifa ya kuchunguzwa kwa ofisa huyo, imetolewa na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Simon Sirro.

IGP Sirro amesema, timu ya kuchunguza video ikimuonesha ofisa wa jeshi hilo akitamka kwamba, Mbowe hatoshinda jimboni humo, kutoka Makao Makuu ya jeshi hilo jijini Dar es Salaam, tayari imetua mkoani humo kwa ajili ya kuanza kazi.

Mbowe ambaye ni mwenyekiti wa chama hicho Taifa, ni mgombea wa jimbo hilo anayetetea kiti chake ambapo video hiyo ilimuonesha akiwa anazozana na ofisa huyo.

Simon Sirro, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP)

Wakati wakizozana,ofisa huyo alimwambia Mbowe “utamshinda yule? huwezi kumshinda, unawadanganya wananchi kuwa utamshinda.”

Video yenye kauli hiyo, ilisambaa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii ikimuonesha ofisa huyo aliyekuwa amevalia sare za polisi, akionesha kukerwa na wananchi kumfuata Mbowe huku akimtaka aingine kwenye gari.

Hata hivyo, Mbowe alimtaka ofisa huyo kutowatimua wafuasi wake waliokuwa wakimfuata.

Awali ofisa huyo alisema “mnafanya watu wanakuja. Ingia kwenye gari tuondoke,”  Mbowe alijibu “sawa, msifukuzie watu wangu, watu wanifuate niwakimbie, hapana!”

Freeman Mbowe, Mwenyekiti Chadema Taifa

Na kisha ofisa huyo akamwambia Mbowe “huwezi kumshinda hata ufanyeje, humshindi, ingia kwenye

gari uondoke, yaani mawazo yako unawadanganya wananchi utamshinda, humshindi.”

IGP Sirro amekiri kuona video hiyo ambapo amesema, timu ya uchunguzi kutoka Makao Makuu ya Jeshi la

Polisi, imekwenda kulichunguza tukio ili kuwa na majibu yanayojitosheleza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!