Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Sheikh Katimba: 28 Oktoba fursa wapinzani kupumua
Habari za Siasa

Sheikh Katimba: 28 Oktoba fursa wapinzani kupumua

Sheikh Rajab Katimba kutoka Taasisi ya na Jumuiya za Kiislamu Tanzania
Spread the love

SHEIKH Rajab Katimba kutoka Taasisi ya na Jumuiya za Kiislamu Tanzania amesema, Uchaguzi Mkuu wa tarehe 28 Oktoba 2020 utumike kama fursa ya upinzani nchini humo kupumua. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Sheikh Katimba amesema hayo leo Jumapili tarehe 27 Septemba 2020 katika uzinduzi wa kampeni za Mgombea Ubunge wa  Kinondoni kupitia chama cha ACT-Wazalendo, Saed Kubenea uliofanyika Viwanja vya Buibui jijini Dar es Salaam.

Amesema, vitendo vya vyama vya upinzani kuhujumiwa katika michakato ya uchaguzi vinapaswa kukomeshwa kwa kuiondoa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) madarakani kupitia uchaguzi huo.

https://youtu.be/YHmWaSZmvI8

“Wapinzani ndio wenye kushughulikiwa,  kuenguliwa wao. Tumeshuhudia mwaka jana wapinzani wamebanwa katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, hii sio fursa ya kuichezea, inatakiwa kila mtu kuitumia kura yake kuhakikisha ufisadi tunauondoa sababu Mungu hapendi ufisadi,” amesema  Sheikh Katimba.

Katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa Novemba 2019, CCM ilishinda uchaguzi huo kwa zaidi ya asilimia 95 baada ya baadhi ya vyama vya upinzani kususia uchaguzi huo kutokana na wagombea wake wengi kuenguliwa kwa sababu mbalimbali ikiwemo kutokidhi masharti ya ujazaji fomu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!