Saturday , 3 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa ACT-Wazalendo yawatumia salamu watakaoiba kura
Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yawatumia salamu watakaoiba kura

Mwenyekiti wa Ngome ya Wazee ya ACT-Wazalendo, Yassin  Mohammed
Spread the love

MWENYEKITI wa Ngome ya Wazee ya ACT-Wazalendo, Yassin  Mohammed amesema, mwenyezi Mungu atawaadhibu watakaoshiriki wizi wa kura kwenye Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020. Anaripoti Faki Sosi …(endelea).

Yassin ameyasema hayo leo Jumapili tarehe 27 Septemba 2020, kwenye uzinduzi wa kampeni za Mgombea Ubunge wa Kinondoni, Saed Kubenea katika Viwanja vya Buibui Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Mzee Yassin amesema, maombi yanayofanya na mtu aliyedhulumiwa hukubaliwa na mwenyezi Mungu haraka.

“Mtu yoyoye atakayedhulumu haki yetu awe ndani ya chama chetu au chama kingine au msimamizi wa uchaguzi mwenyezi Mungu atamuadhibu,” amesema Yassin.

Wakati huo huo, Yassin amewataka wananchi wa Kinondoni kutochagua viongozi wanaotokana na Chama Cha Mapinduzi (CCM), kwa kuwa hawaweki maslahi ya wananchi mbele badala yake wanailinda Serikali .

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!