Thursday , 18 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ACT-Wazalendo yawatumia salamu watakaoiba kura
Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yawatumia salamu watakaoiba kura

Mwenyekiti wa Ngome ya Wazee ya ACT-Wazalendo, Yassin  Mohammed
Spread the love

MWENYEKITI wa Ngome ya Wazee ya ACT-Wazalendo, Yassin  Mohammed amesema, mwenyezi Mungu atawaadhibu watakaoshiriki wizi wa kura kwenye Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020. Anaripoti Faki Sosi …(endelea).

Yassin ameyasema hayo leo Jumapili tarehe 27 Septemba 2020, kwenye uzinduzi wa kampeni za Mgombea Ubunge wa Kinondoni, Saed Kubenea katika Viwanja vya Buibui Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Mzee Yassin amesema, maombi yanayofanya na mtu aliyedhulumiwa hukubaliwa na mwenyezi Mungu haraka.

“Mtu yoyoye atakayedhulumu haki yetu awe ndani ya chama chetu au chama kingine au msimamizi wa uchaguzi mwenyezi Mungu atamuadhibu,” amesema Yassin.

Wakati huo huo, Yassin amewataka wananchi wa Kinondoni kutochagua viongozi wanaotokana na Chama Cha Mapinduzi (CCM), kwa kuwa hawaweki maslahi ya wananchi mbele badala yake wanailinda Serikali .

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

error: Content is protected !!