Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema kuwafuta machozi watumishi wa umma
Habari za Siasa

Chadema kuwafuta machozi watumishi wa umma

Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) nchini Tanzania kimeahidi kulipa malimbikizo ya madeni ya watumishi wa umma pamoja na kuwaongezea mishahara. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mbulu … (endelea).

Ahadi hiyo imetolewa jana Jumatano tarehe 16 Septemba 2020 na Mgombea mwenza wa urais wa Tanzania wa Chadema, Salum Mwalimu wakati akizungumza katika kampeni chauchaguzi huo wilayani Mbulu Mkoa wa Manyara.

Mwalimu alisema, Chadema kikifanikiwa kushinda uchaguzi huo, Serikali yake itapeleka bajeti ya nyongeza bungeni kwa ajili ya kuongeza mishahara ya watumishi wa umma na kuwapandisha madaraja.

Akikazia hoja hiyo, Mwalimu alisema, Serikali ya Chadema italipa fedha za watumishi wote wa umma waliohamishwa vituo vya kazi bila kulipwa stahiki zao.

“Tunafahamu kuna watumishi wa umma waliohamishwa vituo vya kazi bila kupewa stahiki zao, Chadema tunasema tutahakikisha kila mtumishi wa umma aliyehamishwa na hakupewa stahiki zake tunakwenda kulipa,” amesema Mwalimu.

Salimu Mwalimu ni mgombea Mwenza wa Tundu Lissu, ambaye amepewa ridhaa ya Chadema kupeperusha bendera yake katika uchaguzi wa kiti cha Urais wa Tanzania.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!