Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema kuwafuta machozi watumishi wa umma
Habari za Siasa

Chadema kuwafuta machozi watumishi wa umma

Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) nchini Tanzania kimeahidi kulipa malimbikizo ya madeni ya watumishi wa umma pamoja na kuwaongezea mishahara. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mbulu … (endelea).

Ahadi hiyo imetolewa jana Jumatano tarehe 16 Septemba 2020 na Mgombea mwenza wa urais wa Tanzania wa Chadema, Salum Mwalimu wakati akizungumza katika kampeni chauchaguzi huo wilayani Mbulu Mkoa wa Manyara.

Mwalimu alisema, Chadema kikifanikiwa kushinda uchaguzi huo, Serikali yake itapeleka bajeti ya nyongeza bungeni kwa ajili ya kuongeza mishahara ya watumishi wa umma na kuwapandisha madaraja.

Akikazia hoja hiyo, Mwalimu alisema, Serikali ya Chadema italipa fedha za watumishi wote wa umma waliohamishwa vituo vya kazi bila kulipwa stahiki zao.

“Tunafahamu kuna watumishi wa umma waliohamishwa vituo vya kazi bila kupewa stahiki zao, Chadema tunasema tutahakikisha kila mtumishi wa umma aliyehamishwa na hakupewa stahiki zake tunakwenda kulipa,” amesema Mwalimu.

Salimu Mwalimu ni mgombea Mwenza wa Tundu Lissu, ambaye amepewa ridhaa ya Chadema kupeperusha bendera yake katika uchaguzi wa kiti cha Urais wa Tanzania.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MJUMBE wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!