Tuesday , 21 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema kuwafuta machozi watumishi wa umma
Habari za Siasa

Chadema kuwafuta machozi watumishi wa umma

Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) nchini Tanzania kimeahidi kulipa malimbikizo ya madeni ya watumishi wa umma pamoja na kuwaongezea mishahara. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mbulu … (endelea).

Ahadi hiyo imetolewa jana Jumatano tarehe 16 Septemba 2020 na Mgombea mwenza wa urais wa Tanzania wa Chadema, Salum Mwalimu wakati akizungumza katika kampeni chauchaguzi huo wilayani Mbulu Mkoa wa Manyara.

Mwalimu alisema, Chadema kikifanikiwa kushinda uchaguzi huo, Serikali yake itapeleka bajeti ya nyongeza bungeni kwa ajili ya kuongeza mishahara ya watumishi wa umma na kuwapandisha madaraja.

Akikazia hoja hiyo, Mwalimu alisema, Serikali ya Chadema italipa fedha za watumishi wote wa umma waliohamishwa vituo vya kazi bila kulipwa stahiki zao.

“Tunafahamu kuna watumishi wa umma waliohamishwa vituo vya kazi bila kupewa stahiki zao, Chadema tunasema tutahakikisha kila mtumishi wa umma aliyehamishwa na hakupewa stahiki zake tunakwenda kulipa,” amesema Mwalimu.

Salimu Mwalimu ni mgombea Mwenza wa Tundu Lissu, ambaye amepewa ridhaa ya Chadema kupeperusha bendera yake katika uchaguzi wa kiti cha Urais wa Tanzania.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!