Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Bashiru alia wapinzani kuiumiza CCM
Habari za Siasa

Dk. Bashiru alia wapinzani kuiumiza CCM

Spread the love

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Bashiru Ally amelalamikia vyama vya upinzani kukichafua chama hicho. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Amesema, kampeni za mwaka huu kuelekea uchaguzi mkuu wa tarehe 28 Oktoba 2020, zina viashiria visivyo vya kawaida na kwamba, mgombea wa chama chake Dk. John Magufuli ndio mlengwa mkuu wa kuchafuliwa.

Akizungumza kwenye kipindi cha Dakika 45 kinachorushwa na Kituo cha Habari cha ITV cha tarehe 14 Septemba 2020, amedai baadhi ya wagombea wa vyama vya upinzani hawajajiandaa.

Amesema, wanasiasa hao hawajajiandaa kufanya kampeni kwa hoja, badala yake wameamua kuchukua uamuzi wa kuichafua CCM na mgombea wake.

“Unajua kampeni za mwaka huu kidogo zina viashiria visivyo vya kawaida kisiasa, kwa maana baadhi ya wanasiasa nadhani hawajajiandaa kufanya kampeni kwa hoja.

“Wameamua kuchukua uamuzi wa kutuchafua na mlengwa mkubwa ni mgombea wetu wa Urais,” amesema Dk. Bashiru.

Dk. Bashiru ametoa wito kwa wanasiasa kutumia mikutano ya kampeni kujibizana kwa hoja, si kuchafua historia ya CCM kwa kuwa wakiendelea, chama hicho hakitanyamaza kimya.

“Sasa wakitokea wanasiasa ambao wanataka kututoa katika misingi hiyo ambayo kwa kweli ni utamaduni mpya, CCM haiwezi ikanyamaza na kwa sababu tuko wengi, nikianza kuwafungulia hao watu wajibu watapotea tu,” amesema Dk. Bashiru.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!