Wednesday , 27 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Magufuli: Wana Muleba msirudie makosa
Habari za Siasa

Dk. Magufuli: Wana Muleba msirudie makosa

Spread the love

DAKTARI John Magufuli, Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), amewataka wananchi wa Kata ya Kasharunga wilayani Muleba, Bukoba kutorudia kosa la kuchagua wagombea wa upinzani. Anaripoti Mwandishi Wetu, Muleba … (endelea).

Dk. Magufuli ambaye ni Rais wa Tanzania anayemaliza muda wake, ametoa kauli hiyo leo tarehe 15 Septemba 2020 wakati anawanadi wagombea wa CCM wilayani humo.

“Nafahamu tulikuja tukawoamba kura na mimi nilipita hapa nikamuomeba kura mgombea ubunge bahati nzuri mlipa wa CCM, nikaomba mumpe diwani wa CCM bahati mbaya mambo hayakwenda hivyo mkasema hapana.

Lakini kwa sababu nchi hii ya demokrasia na sisi ni wavumilivu tukasema mtoto akikosea haumkati mkono mtu akifanya makosa husamehewa,” amesema Rais Magufuli.

Mgombea huyo wa CCM katika nafasi ya Urais amesema kutokana na msamaha huo, aliamua kutoa kiasi cha Sh. 500 Mil. kwa ajili ya kujenga Hospitali.

“Nilipoletewa bajeti kwenye kata hii inataka hospitali nilitoa Mil. 500 nikajenga hospitali, nasikia aliyekuwa diwani hapa alisema alileta yeye,” amesema Dk. Bashiru.

Aidha, Rais Magufuli amesema aliamua kujenga hospitali hiyo kwa sababu aliona wananchi wanateseka ilhali walimchagua kuwa rais na Mbunge wa Muleba Kusini, Anna Tibaijuka, katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

“Tuliamua tujenge hii hospitali sababu wananchi tuliona wanateseka lakini walimchagua Tibaijuka na mimi huwezi kumhukumu kwa kosa dogo watoto wateseke, pamoja na maji tatizo tulianza kuleta hospitali, lakini katika miaka mitano ijayo tutaleta maji,” amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli amewaomba wananchi wa Kasharunga kuwachagua wagombea wa CCM katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.

“Kosea njia, kosea kuoa au kuolewa unaweza kutoa talaka au kukataa mume lakini usikosee kuchagua, saa nyingine mnanipa shida kusaidia jimbo unakuta diwani ukisema CCM oye anakunyooshea vidole viwili, amesema Rais Magufuli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

Habari za SiasaTangulizi

Mgawo wa umeme: Rais Samia ampa miezi sita bosi mpya TANESCO

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amempa miezi sita Mkurugenzi...

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

error: Content is protected !!