Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Bashiru alia wapinzani kuiumiza CCM
Habari za Siasa

Dk. Bashiru alia wapinzani kuiumiza CCM

Spread the love

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Bashiru Ally amelalamikia vyama vya upinzani kukichafua chama hicho. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Amesema, kampeni za mwaka huu kuelekea uchaguzi mkuu wa tarehe 28 Oktoba 2020, zina viashiria visivyo vya kawaida na kwamba, mgombea wa chama chake Dk. John Magufuli ndio mlengwa mkuu wa kuchafuliwa.

Akizungumza kwenye kipindi cha Dakika 45 kinachorushwa na Kituo cha Habari cha ITV cha tarehe 14 Septemba 2020, amedai baadhi ya wagombea wa vyama vya upinzani hawajajiandaa.

Amesema, wanasiasa hao hawajajiandaa kufanya kampeni kwa hoja, badala yake wameamua kuchukua uamuzi wa kuichafua CCM na mgombea wake.

“Unajua kampeni za mwaka huu kidogo zina viashiria visivyo vya kawaida kisiasa, kwa maana baadhi ya wanasiasa nadhani hawajajiandaa kufanya kampeni kwa hoja.

“Wameamua kuchukua uamuzi wa kutuchafua na mlengwa mkubwa ni mgombea wetu wa Urais,” amesema Dk. Bashiru.

Dk. Bashiru ametoa wito kwa wanasiasa kutumia mikutano ya kampeni kujibizana kwa hoja, si kuchafua historia ya CCM kwa kuwa wakiendelea, chama hicho hakitanyamaza kimya.

“Sasa wakitokea wanasiasa ambao wanataka kututoa katika misingi hiyo ambayo kwa kweli ni utamaduni mpya, CCM haiwezi ikanyamaza na kwa sababu tuko wengi, nikianza kuwafungulia hao watu wajibu watapotea tu,” amesema Dk. Bashiru.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!