Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Membe kutua Tanzania, asema yuko imara
Habari za Siasa

Membe kutua Tanzania, asema yuko imara

Spread the love

BERNARD Kamilius Membe, mgombea urais wa Tanzania kupitia chama cha ACT-Wazalendo, anarejea nchini mwake kesho Jumanne tarehe 15 Septemba 2020 akitokea Dubai. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea)

Membe aliondoka nchini Tanzania hivi karibuni kwenda Dubai ikiwa ni siku chache kupita tangu alipozindua kampeni zake za urais mkoani Lindi na kufanya mikutano kadhaa mikoa ya Mtwara na Pwani.

Mwanadiplosia huyo mashuhuri aliyepata kuwa waziri wa mambo ya nje wa Tanzania kuanzia mwaka 2007 hadi 2015, ametumia ukaunti yake ya Twitter kuelezea safari yake.

“Wana ACT- Wazalendo na Watanzania wenzangu wote! kesho Jumanne ya tarehe 15 Sept.saa 8.40 mchana, nitatua DSM nikitokea Dubai na nitafanya Press Conference Airport.”

“Afya yangu imeimarika na sasa nipo tayari kwa kampeni ya Urais inayoanzia Tabora wiki hii hadi 26 Oktoba 26,” ameandika Membe ambaye pia ni Mshauri Mkuu wa ACT-Wazalendo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!