Saturday , 3 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Membe kutua Tanzania, asema yuko imara
Habari za Siasa

Membe kutua Tanzania, asema yuko imara

Spread the love

BERNARD Kamilius Membe, mgombea urais wa Tanzania kupitia chama cha ACT-Wazalendo, anarejea nchini mwake kesho Jumanne tarehe 15 Septemba 2020 akitokea Dubai. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea)

Membe aliondoka nchini Tanzania hivi karibuni kwenda Dubai ikiwa ni siku chache kupita tangu alipozindua kampeni zake za urais mkoani Lindi na kufanya mikutano kadhaa mikoa ya Mtwara na Pwani.

Mwanadiplosia huyo mashuhuri aliyepata kuwa waziri wa mambo ya nje wa Tanzania kuanzia mwaka 2007 hadi 2015, ametumia ukaunti yake ya Twitter kuelezea safari yake.

“Wana ACT- Wazalendo na Watanzania wenzangu wote! kesho Jumanne ya tarehe 15 Sept.saa 8.40 mchana, nitatua DSM nikitokea Dubai na nitafanya Press Conference Airport.”

“Afya yangu imeimarika na sasa nipo tayari kwa kampeni ya Urais inayoanzia Tabora wiki hii hadi 26 Oktoba 26,” ameandika Membe ambaye pia ni Mshauri Mkuu wa ACT-Wazalendo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!