Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Wawili wadakwa wakijifanya maofisa usalama, polisi
Habari Mchanganyiko

Wawili wadakwa wakijifanya maofisa usalama, polisi

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa
Spread the love

WATU wawili wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam nchini Tanzania kwa tuhuma za kujifanya maofisa wa usalama wa Taifa, Polisi na Mamalaka ya Mapato Tanzania (TRA), kisha kutapeli Sh.35 milionil. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumamosi tarehe 12 Septemba 2020 na Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Jeshi la Polisi wa Kanda hiyo, wakati anazungumza na wanahabari jijini humo.

Kamanda Mambosasa amesema, mtuhumiwa wa kwanza ni Patrick Tarimo, aliyetapeli Sh.20 milioni kwa raia wa kigeni baada ya kujifanya Afisa Usalama wa Taifa.

“Mtuhumiwa huyo, mnamo tarehe 10 Agosti 2020 alitapeli kiasi hicho cha fedha kutoka kwa raia wa kigeni ambapo alimkamata na kujitambulisha yeye ni afisa usalama wa taifa na kufanikiwa kupata kiasi hicho cha fedha,” amesema Kamanda Mambosasa.

Mtuhumiwa wa pili ni, Castory Wambura, aliyejifanya Ofisa wa Polisi na TRA kisha kutapeli Sh.15 milioni wafanyabiashara watano wa Kariakoo.

“Mnamo tarehe 21 Agosti 2020 mtuhumiwa alitapeli kiasi hicho cha fedha kutoka kwa wafanyabiashara watano ambapo alijitambulisha yeye ni Ofisa wa Polisi na TRA,” amesema Kamanda Mambosasa.

Kamanda Mambosasa amesema, watuhumiwa wote wanaendelea kuhojiwa na upelelezi utakapokamilika watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!