Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wawili wadakwa wakijifanya maofisa usalama, polisi
Habari Mchanganyiko

Wawili wadakwa wakijifanya maofisa usalama, polisi

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa
Spread the love

WATU wawili wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam nchini Tanzania kwa tuhuma za kujifanya maofisa wa usalama wa Taifa, Polisi na Mamalaka ya Mapato Tanzania (TRA), kisha kutapeli Sh.35 milionil. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumamosi tarehe 12 Septemba 2020 na Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Jeshi la Polisi wa Kanda hiyo, wakati anazungumza na wanahabari jijini humo.

Kamanda Mambosasa amesema, mtuhumiwa wa kwanza ni Patrick Tarimo, aliyetapeli Sh.20 milioni kwa raia wa kigeni baada ya kujifanya Afisa Usalama wa Taifa.

“Mtuhumiwa huyo, mnamo tarehe 10 Agosti 2020 alitapeli kiasi hicho cha fedha kutoka kwa raia wa kigeni ambapo alimkamata na kujitambulisha yeye ni afisa usalama wa taifa na kufanikiwa kupata kiasi hicho cha fedha,” amesema Kamanda Mambosasa.

Mtuhumiwa wa pili ni, Castory Wambura, aliyejifanya Ofisa wa Polisi na TRA kisha kutapeli Sh.15 milioni wafanyabiashara watano wa Kariakoo.

“Mnamo tarehe 21 Agosti 2020 mtuhumiwa alitapeli kiasi hicho cha fedha kutoka kwa wafanyabiashara watano ambapo alijitambulisha yeye ni Ofisa wa Polisi na TRA,” amesema Kamanda Mambosasa.

Kamanda Mambosasa amesema, watuhumiwa wote wanaendelea kuhojiwa na upelelezi utakapokamilika watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!