Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Profesa Lipumba: Tukipoteza uchaguzi huu, tutajuta
Habari za Siasa

Profesa Lipumba: Tukipoteza uchaguzi huu, tutajuta

Spread the love

PROFESA Ibrahim Lipumba, Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama cha Wananchi (CUF) amesema, wananchi wakishindwa kuutumia Uchaguzi Mkuu wa tarehe 28 Oktoba 2020 kuleta mabadiliko, watajuta kuipoteza nafasi hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Morogoro … (endelea).

Prof. Lipumba ametoa kauli hiyo leo Jumamosi tarehe 12 Septemba 2020 wakati anazungumza na wanahabari mkoani Morogoro, kuhusu mchakato wa uchaguzi huo.

“Uchaguzi huu ni mgumu sana sababu mgombea wa CCM ameonesha suala la ujenzi wa demokrasia na katiba mpya yenye msingi wa demokrasia sio kipaumbele chake, tukiipoteza nafasi hii tutajuta sababu maendeleo yetu ya demokrasia yatarudi nyuma,” amesema Prof. Lipumba.

Wakati huo huo, Prof. Lipumba amewaomba wananchi kuutumia uchaguzi huo, kuchagua viongozi wenye nia ya kuleta katiba mpya na misingi ya demokrasia.

Mwenyekiti huyo wa CUF amesema, harakati za kudai Katiba mpya na misingi mizuri ya demokrasia sio kazi ya viongozi wa kisiasa peke yake, bali ni jukumu la wananchi kuchagua viongozi watakaoleta mabadiliko.

“Ni muhimu sana katika suala la kupata katiba yenye misingi mizuri ya demokrasia sio suala la viongozi peke yao ni suala la wananchi tuweze kujitokeza tulete mabadiliko, tujitokeze katika uchaguzi huu ili tuweze kupata haki,” amesema Prof. Lipumba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!