Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Michezo KMC yaanza kwa kishindo ligi kuu, Kagera yapigwa
Michezo

KMC yaanza kwa kishindo ligi kuu, Kagera yapigwa

Spread the love

TIMU ya KMC FC ya Kinondoni jijini Dar es Salaam imeanza kwa kushindo Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara 2020/21 kwa kuifunga Mbeya City 4-0. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo huo umechezwa leo Jumatatu tarehe 7 Septemba 2020 katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Ushindi huo wa KMC ni mkubwa katika mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo ilianza jana Jumapili kwa michezo saba kati ya tisa.

Katika mchezo mwingine kati ya Kagera Sugar dhidi ya JKT Tanzania katika Uwanja wa Kaitaba, Bukoba mkoani Kagera ulimalizika kwa wenyeji kulala kwa bao moja lililofungwa dakika ya 16 na Adam Adam.

Saa 1:00 usiku wa leo, Azam itacheza na Polisi Tanzania katika Uwanja wa Azam Complex Chamanzi jijini Dar es Salaam kukamilisha mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

error: Content is protected !!