TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) itamfikisha mahakamani mwalimu, Kondwani Masata akituhumiwa kutoa rushwa ya Sh.90,000 kama kishawishi kwa Katibu Tawala Mkoa wa Tabora ili aweze kuhamishiwa Manispaa ya Tabora. Anaripoti Mwandishi Wetu, Tabora … (endelea).
Taarifa iliyotolewa leo Jumatatu tarehe 7 Septemba 2020 na Mkuu wa Takukutu Mkoa wa Tabora, Mussa Chaulo imesema, mwalimu huyo Kondwani Masata wa shule ya sekondari Kizengi Kata ya Kizengi wilayani Uyui Mkoa wa Tabora.
Chaulo amesema, mwalimu huyo atafikishwa mahakamani leo Jumatatu kutokana na tuhuma hizo ambapo walibaini mtuhumiwa aliomba uhamisho na kwa nyakati tofauti amekuwa akishawishi kwa njia ya ujumbe mfupi wa simu (sms) na baadaye kutoa fedha kiasi hicho.
Pia, Takukuru itamfikisha mahakamani, Fidelis Myovella, mhasibu wa Chuo cha Ualimu Tabora na Joseph Kaizerege, mfanyakazi katika manispaa ya Tabora kwa kosa la kutumia nyaraka kumdanganya mwajiri.
Taarifa yote ya Chaulo hii hapa chini;
Leave a comment