Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rungwe ateuliwa kugombea urais Tanzania
Habari za Siasa

Rungwe ateuliwa kugombea urais Tanzania

Hashim Rungwe wa chana cha Chaumma kugombea urais wa Tanzania akirudisha fomu za kuwania kiti hicho
Spread the love

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imemteua Hashim Rungwe wa chana cha Chaumma kugombea urais wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano 28 Oktoba 2020. Rungwe amekuwa mgombea wa 12 kuteuliwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Rungwe ameteuliwa leo Jumanne tarehe 28 Oktoba 2020 na Mwenyekiti wa NEC, Jaji Semistocles Kaijage katika ofisi za tume hiyo jijini Dodoma.

Rungwe amekuwa mgombea wa 12 kati ya 17 waliochukua fomu, kurejesha na kuteuliwa na tume hiyo.

Kati ya wagombea hao 12, wawili ni wanawake ambao ni; Qeen Cuthbert Sendiga wa chama cha ADC na Cecilia Mwanga wa chama cha Demokrasia Makini.

Wagombea wengine waliokwisha rejesha fomu na kuteuliwa ni; Rais John Pombe Magufuli (CCM), Leopard Mahona (NRA), John Shibuda (Ada Tadea), Mutamwega Mgaiwa (SAU), Yeremia Maganja (NCCR-Mageuzi), Ibrahim Lipumba (CUF), Philip John Fumbo (DP), Twalib Ibrahim Kadege (UPDP) na Bernard Membe wa ACT-Wazalendo.

Baadhi ya vyama ambavyo havijarejesha fomu ni vitano, Chadema, AAFP na CCK.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online, MwanaHALISI TV na mitandao yetu ya kijamii kwa taarifa na habari mbalimbali

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!