Monday , 6 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wagombea 10 waliochukua fomu urais Tanzania 
Habari za SiasaTangulizi

Wagombea 10 waliochukua fomu urais Tanzania 

Cecilia Augustino Mwanga wa Demokrasia Makini
Spread the love

WAGOMBEA kumi wa urais wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020 wamechukua fomu Tume ya Taifa ya Uchaguzi  (NEC). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Fomu hizo zimeanza kutolewa tarehe 5 Agosti, 2020  Ofisi za NEC zilizopo nje kidogo ya Jiji la Dodoma eneo la Njedengwa na Mwenyekiti wa tume hiyo, Jaji mstaafu Semistocles Kaijage.

Shughuli ya uchukuaji na urejeshaji wa fomu hizo, utahitimishwa tarehe 25 Agosti 2020, siku ambayo NEC itawateua waliokidhi vigezo vya kuteuliwa.

Hadi kufikia leo Jumamosi tarehe 8 Agosti, 2020, wagombea kumi wamekwisha kuchukua fomu hizo kati yao wanawake ni wawili.

Vyama vilivyochukua fomu hizo ni;  Seif Maalim Seif (AAFP) na mgombea mwenza, Rashid Ligania Rai, Leopard Mahona wa NRA, Philip John Fumbo wa DP,  Rais John Pombe Magufuli wa CCM na mgombea mwenza, Samia Suluhu Hassan na Tundu Lissu wa Chadema na mgombea mwenza, Salum Mwalimu

Wengine ni; Mutamwega Bati Mgaiwa wa SAU,  Qeen Cuthbert Sendiga wa ADC, Twalib Ibrahim Kadege kupitia UPDP, Cecilia Augustino Mwanga wa Demokrasia Makini, Bernard Membe wa ACT- Wazalendo  na mgombea mwenza wake, Profesa Omar Fakih Hamad.

Qeen Cuthbert Sendiga-ADC
Tundu Lissu-Chadema
Bernard Membe-ACT-Wazalendo
Dk. John Magufuli-CCM
Leopard Mahona-NRA
Seif Maalim Seif (AAFP)
Philip John Fumbo-DP
Mutamwega Bati Mgaiwa wa SAU
Twalib Ibrahim Kadege (kulia)-UPDP

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online, MwanaHALISI TV na mitandao yetu ya kijamii kwa habari na taarifa mbalimbali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!