Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa NEC kuanza kutoa fomu za urais leo
Habari za Siasa

NEC kuanza kutoa fomu za urais leo

Spread the love

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) inaanza kutoa fomu za uteuzi kwa wagombea urais wa Tanzania na makamu wake, kuanzia leo Jumatano tarehe 5 -25 Agosti 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa ya NEC imeeleza, fomu hizo zitatolewa ofisi za tume hiyo Njedengwa jijini Dodoma.

Uteuzi wa nafasi hizo itakuwa tarehe 25 Agosti 2020 ofisi za NEC, Dodoma.

Pia, fomu za uteuzi kwa wagombea ubunge, zitatolewa tarehe 12-25 Agosti 2020 katika ofisi za halmashauri nchini.

Fomu za udiwani zitatolewa tarehe 12-25 Agosti 2020 katika ofisi za kata husika.

Kampeni zitafanyika kuanzia tarehe 26 Agosti 2020 hadi 27 Oktoba 2020 na uchaguzi mkuu utafanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020.

Semistocles Kaijage, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Tanzania (NEC)

Tayari vyaka mbalimbali vya siasa nchini vimepitisha wagombea urais ndani ya vyama vyao ili kushiriki uchaguzi huo.

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimempitisha Rais John Pombe Magufuli na mgombea wake mwenza ni, Samia Suluhu Hassan.

Tundu Lissu, amepitishwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) huku Salum Mwalimu akipitishwa kama mgombea mwenza.

Wengine ni; John Shibuda wa Ade-Tadea, Profesa Ibrahim Lipumba wa Chama Cha Wananchi (CUF) na Hashim Rungwe wa Chaumma.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!