Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kifo cha Mkapa, Chadema yaahirisha mikutano kuwapata wagombea urais
Habari za Siasa

Kifo cha Mkapa, Chadema yaahirisha mikutano kuwapata wagombea urais

Spread the love

CHAMA Kikuu cha Upinzani nchini Tanzania, Chadema kimetangaza kuahirisha mikutano yake iliyokuwa ianze tarehe 27 hadi 29 Julai 2020 ili kupisha maombolezo ya kifo cha Rais mstaafu wa awamu ya tatu wa nchi hiyo, Benjamin William Mkapa. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mkapa alifikwa na mauti usiku wa kuamkia jana Ijumaa tarehe 24 Julai 2020 katika moja ya Hospitali jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu.

Mwili wake, utaanza kuagwa kesho Jumapili tarehe 26 hadi 28 Julai 2020 katika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam kisha utasafirishwa kwenda kijijini Lupasa, Masasi Mkoa wa Mtwara Jumatano tarehe 29 Julai 2020.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumamosi tarehe 25 Julai 2020 makao makuu ya Chadema, Kinondoni jijini Dar es Salaam, Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Bara, Benson Kigaila amesema, mikutano hiyo imesogezwa mbele ili kutoa fursa ya Watanzania kuomboleza kifo cha Rais mstaafu Mkapa.

Akitangaza mabadiliko ya ratiba, Kigaila amesema, kikao cha kamati kuu kilikuwa kikutane tarehe 27 Julai 2020 sasa kitafanyika Agosti 2, 2020. Baraza Kuu tarehe 28 Julai 2020, kimesogezwa mbele hadi Agosti 3, 2020 na mkutano mkuu uliokuwa ufanyike tarehe 29 Julai 2020 sasa utafanyika tarehe 4 Agosti 2020.

Amesema, mikutano hiyo yote itafanyikia ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam ikiwa na lengo la kujadili masuala mbalimbali hususan kuwapata wagombea urais wa Tanzania na Zanzibar katika Uchaguzi Mkuu tarehe 28 Oktoba 2020.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online na MwanaHALISI TV kwa habari mbalimbali. Pia tembelea mitandao yetu ya kijamii ya Twitter, Facebook na Instagram

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari za Siasa

Wizara ya Kilimo yapanga kutumia Sh. 1.2 trilioni 2024/25

Spread the loveWIZARA ya Kilimo, imepanga kutumia bajeti ya Sh. 1.2 trilioni...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaanza msako wanaotoa mikopo kausha damu

Spread the loveSERIKALI imeanza kufuatilia watu, vikundi na taasisi zinazotoa kinyume cha...

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

error: Content is protected !!