Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mhariri MwanaHALISI apenya kura za maoni Z’bar
Habari za Siasa

Mhariri MwanaHALISI apenya kura za maoni Z’bar

Jabir Idrissa
Spread the love

JABIR Idrissa, aliyekuwa Mhariri wa Gazeti la MwanaHALISI, ameshinda kura za maoni za ubunge kupitia Chama cha ACT-Wazalendo katika Jimbo la Pangawe, Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja. Anaripoti Mwandishi Wetu, Unguja … (endelea).

Jabir aliyekuwa mmoja wa waajiriwa wa Kampuni ya Hali Halisi Publishers Ltd (HHPL), iliyokuwa ikizalisha magazeti ya MwanaHALISI, Mseto na Mawio amepata kura 41 dhidi ya mpinzani wake Hamad Ali Hamad aliyepata kura 36. Bahamadi alikuwa mbunge wa Magogoni, mjini Zanzibar mwaka 2010-2015.

Washindani wengine kwenye kura hizo walikuwa Aminie Mohamed Juma aliyepata kura 20 na Juma Khelef Juma aliyepata kura tano kati ya kura 103, kura moja iliharibika.

Jabir alianza kuitumikia Kampuni ya HHPL mwaka 2006 akitokea gazeti la Mtanzania.

Magazeti la MwanaHALISI, Mseto na MAWIO yamefungwa na serikali kwa kudaiwa kufanya uchochezi. Jabir alijiunga na chama hicho visiwani Zanzibar mwaka jana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!