Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Watia nia wafutiwa mishahara
Habari za Siasa

Watia nia wafutiwa mishahara

Spread the love

SERIKALI imeagiza kwamba, watumishi wa umma waliotia nia ya kugombea nafasi mbalimbali za kisiasa, wasilipwe mishahara yao. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Barua hiyo imetolewa na Ofisi ya Msajili wa Hazina tarehe 21 Julai 2020, likiwataka wakurugenzi na wakuu wote wa taasisi kuhakikisha, watumishi hao hawalipwi mishahara hiyo kuanzia Julai 2020.   

Neema Msonda, Msajili wa Hazina pia amewataka wakuu wa taasisi hizo kuandaa na kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa maelekezo hayo ifikapo tarehe 25 Julai 2020.

“Maelekezo haya ya kutolipa mshahara wa mwezi Julai, yanawahusu watumishi waliopatiwa vibali/ruhusa na waajiri wao pamoja na watumishi waliogombea bila vibali kutoka kwa waajiri wao au kupitia mamlaka stahiki,” imeeleza barua hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!