ISSA Mtemvu, ameibuka mshindi kura za maoni za Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jimbo la Kibamba, Dar es Salaam kwa kupata kura 83 kati ya 369. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).
Mkutano wa kura za maoni umefanyika leo Jumanne tarehe 21 Julai 2020 katika ukumbi wa Victorius Genesis, Kimara Temboni, Dar es Salaam.
Issa ni mdogo wake na Abbas Mtemvu ambaye naye ameongoza kura za maoni jimbo la Temeke, Dar es Salaam.
Katika matokeo hayo ya Kibamba, Vicky Kamata, Mbunge Viti Maalum anayemaliza muda wake, ameshika nafasi ya pili akipata kura 49 huku Mwesigwa Siraji akishika nafasi ya tatu kwa kura 36.
Wagombea waliochukua fomu walikuwa 176 lakini waliorejesha walikuwa 170 ambao wote kwa pamoja walijinadi kwa wajumbe wa mkutano huo ili waweze kuwapigia kura.
Katika hatua nyingine, Mbunge anayemaliza muda wake wa Kalenda Mkoa wa Iringa, Godfrey Mgimwa ameshindwa kura za maoni kwa kupata kura saba.
Aliyoongoza ni Jackson Kiswaga aliyepata kura 221 akifuatiwa na Leo Martin Mavika kura 149 na Bryson Kibasa kura 33. Wapiga kura walikuwa 589.
Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online na MwanaHALISI TV kwa habari mbalimbali
Leave a comment