Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Tangulizi Magufuli athibitishwa kwa asilimia 100 kugombea urais Tanzania
Tangulizi

Magufuli athibitishwa kwa asilimia 100 kugombea urais Tanzania

Spread the love

WAJUMBE wa Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamemthibitisha Dk. John Pombe Magufuli kuwa mgombea Urais wa Tanzania kwa asilimia 100 katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Shughuli hiyo ya upigaji kura imefanyika leo Jumamosi tarehe 11 Julai 2020 jijini Dodoma.

Akitangaza matokeo hayo, Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai amesema, wajumbe wa mkutano huo ni 1822 na waliopiga kura walikuwa 1822.

Spika Ndugai amesema, hakuna kura hata moja iliyoharibika.

Amesema, kura halali zilikuwa 1822, “kura halali ni 1822. Kura za ndiyo ni 1822 ambayo ni sawa na asilimia 100 ya kura zote. Hakuna kura ya hapana.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

error: Content is protected !!