Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge CCM ahojiwa kwa ‘kugawa’ rushwa
Habari za Siasa

Mbunge CCM ahojiwa kwa ‘kugawa’ rushwa

Spread the love

TAASISI ya Kuzia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), imemuhoji Lingstone Lusinde, aliyekuwa Mbunge wa Mtera (CCM) kwa tuhuma za kugwa rushwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Kwa mujibu wa Sosthenes Kibwengo, Mkuu wa Takukuru mkoani Dodoma, Lusinde alifikishwa katika ofisi za taasisi hiyo zilizoko wilayani Chamwino, Jumatano tarehe 8 Julai 2020.

Kibwengo amesema, Takukuru ilimuita na kumuhoji Lusinde, baada ya kupata taarifa ya kwamba, wajumbe wa vikao vya uteuzi wa wagombea wa CCM nyumbani kwake, kwa minajili ya kuwapa fedha kama kishawishi ili wampitishe kugombea katika uchaguzi huo.

Kibwengo amesema, baada ya mwanasiasa huyo kuhojiwa, aliachiwa na kuwamba uchunguzi juu ya sakata hilo unaendelea.

“Tulipata taarifa ya kwamba anakusanya wapigakura nyumbani kwake awapatie fedha kama kishawishi. Jana tulimhoji ofisini kwetu Chamwino, na kisha tuliamuachia. Lakini uchunguzi unaendelea,” amesema Kibwengo.

Lusinde alikuwa mbunge wa Mtera kwa vipindi viwili mfululizo, kuanzia mwaka 2010-2015 hadi 2015-2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!