Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Sheikh Ponda ataja sifa za wagombea uchaguzi mkuu
Habari za Siasa

Sheikh Ponda ataja sifa za wagombea uchaguzi mkuu

Sheikh Ponda Issa Ponda (katikati)
Spread the love

SHEIKH Ponda Issa Ponda, Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam Tanzania, ametaja sifa za wagombea katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 2020. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 9 Julai 2020, jijini Dar es Salaa amesema, waraka wa taasisi hiyo uliotolewa leo umeorodhesha sifa ambazo mgombea kwenye ngazi mbalimbali anapaswa kuwa nazo.

Ametaja sifa zilizoelezwa kwenye waraka huo kuwa ni:-

1. Mgombea awe mkweli na mwenye utu.

2. Awe mwenye kuheshimu kiapo.

3. Awe mwenye sifa ya kupiga vita ubaguzi wa aina zote.

4. Awe na elimu kubwa au wastani, mwenye maarifa ya kutosha ya kuongoza watu na serikali.

5. Awe mtu mwenye mtazamo wa maendeleo kwa Taifa na Watanzania wote.

6. Awe mwenye kuheshimu Uhuru wa Mawazo ya watu wengine.

7. Awe mwenye kuzijua Haki za binaadamu na kuzilinda.

8. Asiwe mwenye kutumia vibaya madaraka na kuvunja sheria za nchi.

9. Awe ni mwenye kupenda Umoja wa Taifa na dhamira ya Muungano wa kweli.

10. Asiwe fisadi na mwenye kuficha ukweli.

11. Awe mwenye kumtambua Mwenyezi Mungu wa Walimwengu wote.

12. Asiwe kibri, dikteta mkandamizaji na mdhalilishaji wa watu anaowaongoza.

13. Asiwe mtu mwenye kujali maslahi yake na kundi lake sambamba na kufikiria sheria za kujilinda dhidi ya mkondo wa sheria kwa tuhuma za ufisadi na uvunjaji wa Haki za Binadamu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

error: Content is protected !!