Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu: Narejea Tanzania kabla ya Julai 28
Habari za SiasaTangulizi

Lissu: Narejea Tanzania kabla ya Julai 28

Tundu Lissu, Makamu Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

TUNDU Antipas Lissu, Makamu mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) amesema, atarejea Tanzania mwishoni mwa mwezi huu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Amesema, atafanya hivyo ili aweze kuhudhuria mkutano wa Baraza Kuu na mkutano mkuu wa chama hicho tarehe 28 na 29 Julai 2020.

Mikutano hiyo, pamoja na mambo mengine, itampitisha mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 2020.

Mchakato wa uchakuaji na urejeshaji fomu za kuwania Urais wa Tanzania unaanza leo Jumamosi tarehe 4 hadi 19,2020.

Wagombea au mawakala wao watakuwa na fursa ya kuchukua fomu kisha kutafuta wadhamini 100 katika kila kanda kumi za chama hicho.

Lissu ni miongoni mwa wanachama ambao wamekwisha tia nia hadharani ya kuwania nafasi hiyo ya juu kabisa ya uongozi wa Taifa hilo lililopo Afrika Mashariki.

Akijojiwa na mwandishi nguli nchini Tanzania, Jenerali Ulimwengu katika kipindi chake kinachorushwa na JeneraliOnline, Lissu amesema, baada ya safari ndefu ya kutibu majeraha na kupona, sasa yuko tayari kurejea nchini humo.

Amesema anarejea ili kuomba ridhaa ya wana Chadema na Watanzania kumchagua kuwa Rais wa Tanzania ili kuwatumikia kwa kuunganisha nguvu kwa pamoja kwani ana imani mtu mmoja pekee hawezi kuongoza nchini.

Tangu tarehe 7 Septemba 2017, Lissu aliposhambuliwa na watu wasiofahamika akiwa nyumbani kwake Area D jijini Dodoma, mwanasiasa huyo amekuwa nje ya Tanzania kwa matibabu.

Siku hiyohiyo usiku, alihamishiwa Hospitali ya Nairobi nchini Kenya kwa matibabu hadi tarehe 6 Januari 2018 alipopelekwa nchini Ubelgiji kwa matibabu zaidi.

Hata hivyo, Lissu mwenyewe amekwisha kusema amepona na hatumii dawa zozote na anachosubiri ni kureja nyumbani Tanzania kuendelea na shughuli zake mbalimbali hasa za kisiasa.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online & MwanaHALISI TV kwa habari zaidi

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!