Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Adakwa na doti 600 vitenge vyenye nembo ya CCM
Habari Mchanganyiko

Adakwa na doti 600 vitenge vyenye nembo ya CCM

Spread the love

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa wa Shinyanga, inamshikilia mfanyabiashara Joseph Tasia akiwa na doti 600 za vitenge vyenye nembo ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Mwandishi Wetu, Shinyanga … (endelea).

Takukuru imesema, vitenge hivyo vya kawaida, vinadaiwa kutaka kutumika kushawishi wapiga kura kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020.

Hayo yamesemwa leo Ijumaa tarehe 3 Julai 2020 na Mkuu wa Takukuru, Mkoa wa Shinyanga Hussein Mussa kupitia taarifa yake kwa umma.

         Soma zaidi:-

Mussa amesema, tarehe 29 Juni 2020 saa 3 usiku, katika mtaa wa Mwasele B nyumba ya Tasia, walimkuta na doti hizo za vitenge vikiwa vimehifadhiwa nyumbani kwake jambo ambalo linaashiria vilikuwa vinaandaliwa kutumika katika kufanya ushawishi kwa wapiga kura.

Amesema, uchunguzi walioufanya, wamebaini, Tasia ambaye ni mfanyabiashara wa usafiri wa magari madogo ‘taxi’ hana duka na wala hafanyi biashara ya kuuza vitenge.

“Katika mahojiano na maafisa wa Takukuru Mkoa wa Shinyanga, ameshindwa kutoa maelezo yanayojitosheleza kuhusiana na mzigo husika na hata nyaraka za manunuzi ya mzigo huo alizowasilisha hazijitoshelezi na hivyo kuongeza mashaka juu ya uhalali wa vitenge hivyo,” amesema Mussa.

Amesema, uchunguzi wa kina bado unaendelea ili kubaini iwapo vitenge vilikuwa ni kwa ajili ya kuhusika na vitendo hivyo vya rushwa katika uchaguzi ujao au ni kwa ajili ya kufanya biashara msimu huu wa kuelekea uchaguzi mkuu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

error: Content is protected !!