Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maharagande ajitosa rasmi ubunge Segerea
Habari za Siasa

Maharagande ajitosa rasmi ubunge Segerea

Spread the love

MBARALA Maharagande, Katibu wa Idara ya Haki za Binadamu Taifa wa Chama cha ACT-Wazalendo, amechukua fomu ya kugombea ubunge wa Segerea jijini Dar es Salaam, katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Maharagande amekabidhiwa fomu hiyo leo Jumatano tarehe 1 Julai 2020 na Athuman Maarufu, Katibu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Jimbo Segerea.

Baada ya kukabidhiwa fomu hiyo, Maharagande amesema, ameanza rasmi safari ya kuliwania jimbo hilo lililokuwa mikononi mwa Chama cha Mapinduzi (CCM), chini ya Bonah Kamoli.

“Safari imeanza rasmi, leo nimechukua fomu ya kugombea ubunge wa Jimbo la Segerea katika mchakato ndani ya chama,” amesema Maharagande.

 Chama cha ACT-Wazalendo kimefungua rasmi pazia la uchukuaji na urejeshaji fomu za kugombea urais ubunge, uwakilishi na udiwani leo, ambapo linatarajia kukoma tarehe 13 Julai mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za Siasa

Askofu Shoo awataka ACT kupigania maslahi ya Taifa, wasikubali kuhongwa

Spread the loveALIYEKUWA Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Askofu...

Habari za Siasa

Biteko aagiza waajiri kudhibiti vifo mahali pa kazi

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!