NAIBU Waziri wa Kilimo nchini Tanzania, Hussein Bashe amepiga marufuku watu waliowekeza kwenye mashamba na majengo ya ushirika kuacha tabia ya kukopea mali za ushirika bila ridhaa ya wanaushirika na Tume ya Ushirika. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kilimanjaro … (endelea).
Bashe ameyasema hayo leo Jumatano tarehe 1 Julai, 2020 wakati alipofanya ziara ya kukagua mashamba makubwa ya wakulima wa mazao mbalimbali ya mahindi na ngano pamoja na kuzungumza na vyama vya ushirika mkoani Kilimanjaro.
Aidha amesema, kumekuwepo na migogoro mbalimbali ya baadhi ya wawekezaji waliowekeza katika mashamba na majengo ya wakulima kukopea mali za wanaushirika hali ambayo imepelekea Serikali kuanza kuhangaika kukomboa mali hizo.
“Ni marufuku kwa nchi nzima hati ya chama cha ushirika mtu yeyote aliyewekeza kwenye shamba la ushirika au jengo la ushirika haruhusiwi kwenda kukopea mali ya ushirika bila ridhaa ya wanaushirika na Tume ya ushirika, kwa sababu tuna kesi nyingi za mali za ushirika zimekopewa, sasahivi Serikali tunahangaika kuzikomboa,” amesema Bashe.
Hata hivyo, amemwagiza mrajisi wa vyama vya ushirika, Dk. Benson Ndyege kuhakikisha anapitia mikataba yote ya wawekezaji waliopo katika mashamba mbalimbali ya vyama vya ushirika wilayani Hai ili kujua utaratibu wa kuwaweka wawekezaji kama ulifatwa.
Mheshimiwa Bashe
Na lile jengo kuuuubwa la Ushirika pale Lumumba linamilikiwa na nani? Na wakulima washirika au na wajanja wachache waliopokonya mali ya wakulima? Tunaomba maelezo