Tuesday , 30 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa DED alivyoomba radhi mara tatu mbele ya JPM
Habari za Siasa

DED alivyoomba radhi mara tatu mbele ya JPM

Asajile Mwambambale, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa akiandika msamaha wake mbele ya Rais John Magufuli
Spread the love

ASAJILE Mwambambale, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Mkoa wa Morogoro (DED), amemuomba radhi mara tatu, Rais John Magufuli, kwa kosa la kutotatua changamoto ya mgogoro wa ardhi  wilayani humo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kilosa … (endelea).

Mwambambale amelazimika kuomba msamaha huo, baada ya kuandamwa na malalamiko ya kutowajibika katika utatuzi wa migogoro, yaliyoibuliwa na wananchi wa wilaya hiyo, leo Jumatatu tarehe 29 Juni 2020, katika ziara ya Rais Magufuli.

Mkurugenzi huyo wa Kilosa alikuwa anatuhumiwa kutosikiliza kero za wananchi kuhusu migogoro ya ardhi, pamoja na kuandika barua iliyokuwa inawakataza wananchi kutotumia mashamba yaliyokuwa yaliyokuwa yameuzwa kinyume cha sheria..

Kufuatia malalamiko hayo, Mwambambale amemuomba radhi Rais Magufuli huku akimuahidi atajirekebisha kwani amekwisha kytambua amejikwaa

“Rais ninaomba unisamehe, mheshimiwa rais ninaomba unisamehe, mheshimiwa rais ninaomba unisamehe,” amesema Mwambambale alipopewa fursa ya kuzungumza mbele ya Rais Magufuli na umati ya wananchi.

“Kuna kazi nyingine umenipa na nimefanya kwa mafanikio, kuna miradi ya maendeleo mbalimbali nimejenga. Najifunza naomba unisiamehe, naomba unipe nafasi ya pili sitokuangusha,” amesema Mwambambale kwa sauti ya unyonge

Kabla ya Mwambambale kuomba toba hiyo, Rais Magufuli alimuuliza Seleman Jaffo, Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI, historia ya utendaji kazi wa mkurugenzi huyo, ambaye alikiri utendaji wake kuwa na dosari, kutokana na malalamiko mengi ya wananchi wa wilaya yake.

“Rais kutoa haki kuna kazi nzito sana, kwa haraka, kwa taarifa ambazo juzi nimepata kutoka kwa mkuuu wa mkoa, kuna eneo liliuzwa hapa. Na mheshimiwa Rais nilikujulisha kuhusu  hili eneo na hili ulilitolea maelekezo kule tulikotoka,” amesema Jaffo na kuongeza:

“Kila mwananchi analalamika kwa upana wake, nadhani ungelitathimini kwa upana jambo hili. Lakini ni fundisho kwa viongozi wengine, kwa nini wananchi wote wanalalamika?  Hili halina afya kabisa kwa nyinyi mliokuwa na dhamana hili jambo sio sawa, malalamiko hayatoi taswira nzuri,” amesema

Baada ya Jaffo kutoa kauli hiyo, Rais Magufuli alimpa onyo mkurugenzi huyo na kumtaka kuandika hadharani barua ya kutengua maamuzi yake ya kuuza mashamba hayo  pamoja na kuwaomba radhi wananchi kwa dosari zilizojitokeza.

“Mkurugenzi hiyo barua uliiandika wewe, andika chini ya barua hii (barua hiyo ya zuio) useme nimefuta mwenyewe na ninaomba msamaha kwa wananchi, kama huwezi kuandika niende na barua zangu nikaamue mimi mwenyewe nitakavyoamua kuandika,” amesema Rais Magufuli.

Mkurugenzi huyo alikubali na kuandika kisha kuirejesha kwa Rais Magufuli ambaye alisema kwa kuwa ameomba msamaha, anasamehewa na kumtaka kujirekebisha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

error: Content is protected !!