Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ‘Meya’ Ubungo atimkia ACT-Wazalendo
Habari za SiasaTangulizi

‘Meya’ Ubungo atimkia ACT-Wazalendo

Ramadhan Kwangaya
Spread the love

RAMADHANI Kwangaya, aliyekuwa Kaimu Meya wa Manispaa ya Ubungo jijini Dar es Salaam amejiunga na chama cha ACT-Wazalendo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kwanganya ambaye alikuwa Diwani wa Manzese kupitia Chama Cha Wananchi (CUF) amechukua uamuzi huo siku chache kupita tangu Baraza la Madiwani wa Manispaa ya Ubungo kuvunjwa.

Taarifa iliyotolewa leo Jumatano tarehe 17 Juni 2020 na Naibu Katibu wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma wa ACT-Wazalendo, Janeth Rithe imesema, Kwanganya amejiunga na chama hicho pamoja na aliyekuwa Diwani wa Viti Maalum (CUF) Manispaa ya Ubungo na Diwani wa Jiji la Dar es Salaam, Leila Madibi.

Kwangaya ambaye alikuwa Naibu Meya wa Manispaa ya Ubungo alikaimu nafasi ya Meya wa Ubungo kuanzia tarehe 12 Mei 2020 baada ya Boniface Jacob kupoteza sifa za kuwa Meya.

Jacob ambaye pia alikuwa Diwani wa Ubungo alipoteza nafasi ya umeya baada ya barua inayoelezwa kuandikwa tarehe 28 Aprili 2020 na katibu wa Chadema Kata ya Ubungo kwenda kwa mkurugenzi wa halmashauri ya Ubungo kuonyesha amevuliwa uanachama hivyo kupoteza sifa za kuwa meya.

Hata hivyo, Jacob mwenyewe, Chadema makao makuu na mtu huyo ambaye jina lake lilitumika kwenye barua hiyo kudai haina ukweli, kwani hakuna kikao chochote kilichokaa cha kumjadili Jacob kisha kumvua uanachama.

Jacob alifikisha suala hilo Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) kuonyesha kutokubaliana na uamuzi wa mkurugenzi wa Ubungo.

Hadi sasa, hakuna kilichoelezwa juu ya rufaa hiyo iliishia wapi kwani si Tamisemi au Jacob waliozungumzia suala hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!