Tuesday , 5 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Kidato cha tano Tanzania kuanza masomo Julai 20
Habari Mchanganyiko

Kidato cha tano Tanzania kuanza masomo Julai 20

Suleiman Jafo, Waziri wa Tamisemi
Spread the love

WAZIRI wa Nchi,Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Selemani Jafo amesema, wanafunzi 73,101 wamechaguliwa kujiunga na kidato cha tano mwaka 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Jafo amesema, wanafunzi hao watatakiwa kuripoti shuleni tarehe 18 Julai 2020 ili kuanza masomo tarehe 20 Julai 2020.

Waziri Jafo ameyasema hayo leo Jumatano tarehe 17 Juni 2020 jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Wanafunzi wa kidato cha sita walipokuwa wanafanya mtihani

Amesema, miongoni mwa wanafunzi waliochaguliwa wanafunzi 1,572 wakiwemo wasichana 685 na wavulana 887 wamechaguliwa kujiunga na shule za vipaji maalumu wakiwamo wanafunzi wanne wavulana wenye mahitaji maalum.

Kwa upande wa vyuo, Waziri Jafo amesema, wanafunzi 9,264 wakiwemo wasichana 4,314 na wavulana 4,950 wamechaguliwa kujiunga na vyuo vya elimu ya ufundi, vyuo vya afya na vyuo vya ualimu katika ngazi ya stashahada.

Waziri Jafo ametoa agizo kwa wanafunzi kuhakikisha wanaripoti katika kipindi cha wiki mbili tangu tarehe ya kufungua shule.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

RPC Songwe awafunda trafki kuzingatia uadilifu

Spread the loveASKARI wa kikosi cha usalama barabarani mkoani Songwe wametakiwa kuendelea...

Habari Mchanganyiko

Mchimba madini jela maisha kwa kubaka, alihonga Sh 500

Spread the loveMahakama ya wilaya ya Songwe imemtia hatiani na kumhukumu kifungo...

Habari Mchanganyiko

Mlima wa Moto wazindua kongamano la SHILO kumuenzi Rwakatare

Spread the loveKANISA la Mlima wa Moto Mikocheni jijini Dar es Salaam,...

Habari MchanganyikoTangulizi

20 wafariki dunia kwa mafuriko Manyara

Spread the loveMVUA za vuli zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimeleta madhara...

error: Content is protected !!